Katika kuhakikisha vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia hasa kwa wanafunzi vinamaliza, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali imesema imejipanga katika kutoa  elimu  ya udhalilishaji na ukatili  kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari Unguja na Pemba.

Mkurugenzi Elimu na Maandalizi kutoka Wizara ya Elmu Zanzibar, Safia Ali Rijali alibainisha hayo visiwani  hapa ikiwamo ni moja ya jitihada za kukabiliana na matendo hayo ambayo yamekuwa ni tishio kubwa hasa kwa watoto wakiwamo wanafunzi.

Alisema mpango huo wa kutoa elimu mashuleni umekuja baada ya kuonekana vitendo hivyo kukithiri , huku kundi la wanafunzi nalo lilikubwa na vitendo hivyo ambavyo baadhi ya wakati hurudisha nyuma jitihada za elimu kwa wanafunzi wanaokumbwa na kadhia hiyo.
  
Alisema lengo kuu la elimu kwa anafunzi ni kuwawezeha kufahamu kwa kina suala au viashia vya udhallishaji na ukatili pamoja na madhara yake, ili kila mwanafunzi kuwa na elimu ya kujikinga navyo pindi akionesha ishara ya vitendo hivyo.

Alisema mbali ya elimu hiyo ya kina kwa wanafunzi mbali mbali lakini pia Wizara imepanga kuanzisha vikundi maalumu vya kutoa elimu ya udhalilishaji ambavyo vitatumika katika kusambaza elimu na kusimamia  udhalilishaji ndani ya Shule.

“Lakini pia tumepanga kuzipa elimu hiyo kamati za Shule zinazosimamia Elimu pamoja na kutoa Elimu kwa walimu katika Shule hizo juu ya namna ya kusimamia matendo hayo ili yasitokee katika shule zetu”alisema.

Hata hivyo alisema katika kipindi cha mwezi miezi sita Januari hadi Juni mwaka jana  Wizara ya Elimu  ilipokea  kesi 30 za udhalilishaji kwa watoto ambapo kesi 10 ambapo Unguja zilikuwa 4 na Pemba 6.

Alisema kwa upande wa kesi za ubakaji zilikuwa 5 ambapo Unguja ilikuwa  kesi 1 na Pemba kesi 4 pamoja na kesi za 11 za  Ujauzito kwa wanafunzi hao ambapo Unguja 8 na Pemba 3.

Kwa upande wa Sheikh Ali Abdallah Amour kutoka Jumuiya ya Maimamu Zanzibar alisema kushamiri kwa vitendo hivyo vya udhalilishaji na ukatili kwa watoto vinatokana na jamii kuacha utamaduni wao na kufuata tamaduni za kigeni.

Alisema umefika wakati sasa kwa wazazi na walezi kuunga kwa pamoja katika kulea watoto kwa kufuata malezi yalio bora hasa kwa kufuata misingi ya dini ili kuwa jamii iliyo bora, huku akibainisha kuwa pindi kila mmoja akifuata njia hiyo ni wazi kwamba vitendo hivyo vinaweza kuondoka.

Kwa Upande wake Mwanaharakati wa kupambana na vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto  Nassor Hamadi alisema kuwa ili vitendo vya ukatili na udhaliliishaji kwa watoto vikomeshwe Zanzibar Serikali haina budi kusimamia Sheria zake.

Alisema nchi ina sheria nzuri sana ambazo zinamlinda mtoto kikubwa kinachokosekana ni kuzisimamia Sheria hizo kwa wale wafanyaji wa matendo hayo ni kuchukulia hatua za haraka.

Imeandikwa na Haji M. Mohd, chini ya ufadhiliwa UNICEF

Facebook Blogger Plugin by Piere

Post a Comment

 
Top