Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC imeandaa rasimu ya mtaala wa elimu ya wapiga kura ambao utatumika kwa taasisi zinazotakutoa elimu ya wapiga kura baada ya kupewa kibali na tume cha kutoa elimu.

Kamishna wa Tume ya Uchaguzi Mhe. JOKHA KHAMIS MAKAME alieeleza hayo katika ukumbi wa mikutano wa Tume hiyo wakati akifungua mkutano wa kujadili rasimu ya mtaala wa Elimu ya Wapiga Kura.

Alisema matayarisho ya Mtaala huo yanatokana na maelekezo ya kifungu cha 106(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar Nam. 4 ya mwaka 2018 yanayoitaka Tume kutayarisha mtaala wa Elimu ya Wapiga Kura utakaotumiwa na Wadau wa Uchaguzi wanaotaka kutoa Elimu ya Wapiga Kura.

Mshauri elekezi JUMA HAJI USSI alisema Tume kwa upande wake inatarajia utekelezaji wa mtaala huo wa elimu utawasaidia wadau wa uchaguzi wakiwemo washirika wa maendeleo, Waangalizi wa Uchaguzi, Vyama vya Siasa na Asasi za Kiraia ambapo lengo la mtaala huo ni kuwajengea uelewa na kuangalia kwa kiasi gani elimu hiyo itawafikia walengwa.

Ndugu Juma alisema   Mtaala huo umeainisha misingi ya utoaji wa elimu ya Wapiga kura pamoja na Sheria ya uchaguzi ya Zanzibar ambayo imetoa mamlaka ya kuratibu, kusimamia, na kuendesha elimu ya Wapiga Kura kwa mujibu wa Sheria ya uchaguzi ya Zanzibar ya Nam. 4 ya mwaka 2018.

Alifahamisha kuwa utayarishaji wa mtaala huo, pia ulifanyika kwa kuzingatia vigezo vya kisheria na ushirikishwaji wa makundi ya kijamii ili umsaidie Mzanzibari kupata elimu bora inayohusu Demokrasia katika masuala ya kiuchaguzi.

Washiriki wa mkutano huo wameipongeza Tume kwa kuandaa mtaala ambao umekidhi vigezo na kuzingatia umuhimu wa makundi mbalimbali katika masuala ya Uchaguzi

Rasimu ya mtaala wa elimu ya Wapiga Kura umeainisha makundi mbali mbali ambayo yanahusika moja kwa moja katika ushiriki na ushirikishwaji wa masuala ya uchaguzi wakiwemo Vyama vya Siasa, Asasi za Kiraia, Makundi Maalum na vyombo vya habari

Facebook Blogger Plugin by Piere

Post a Comment

 
Top