Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jaji Mkuu Mstaafu Hamid Mahmoud Hamid amewataka wale wote waliokuwa hawana vitambulisho vipya vya mzanzibar mkaazi,kufanya hima ya kuvifatilia vitambulisho hivyo ili kuwa na sifa ya kuandikishwa pamoja na kufanyiwa uhakiki katika daftari la kudumu la wapiga kura.


Jaji Hamid alitoa kauli hiyo katika ziaza yake ya kutembelea vituo vya zoezi la uandikishaji pamoja uhakiki katika daftari la kudumu la wapiga kura huko Wilaya ndogo ya Tumbatu Mkoa Kusini Unguja.

Alisema ni jambo na busara kwa wale ambao hawana vitambulisho vipya vya mzanzibar vilivyofanyiwa uhakiki, kufanya uharaka wa kwenda kuvitafuta vipya ili kutumia fursa yao ya kisheria ya kuandikishwa pamoja na kufanyiwa uhakiki katika daftari la wapiga kura.

Alisema tume inaendelea na kazi yake ya kufanya ya uandikishaji wa wapiga kura wapya na uhakiki wa taarifa za wapiga katika Wilaya mbali mbali kwa kuwahusisha wale tu waliopata vitambulisho vipya vya mzinzibar mkaazi, huku akisisitiza kuwa kwa wale ambao hawana vitambulisho vipya bado wana fursa ya kuandikishwa pindi kiwavipata vitambulisho hivyo.

Hata hivyo alisema Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) baada ya kukamilika kwa zoezi hilo itafanya tathmini ili kuangalia kwa namna ambavyo itaweza kusaidia kuzitatua changamoto za Wananchi ambao watakosa fursa ya kuandikishwa katika Daftari kutokana na sababu ya kukosa Vitambulisho vya Mzanzibar Mkaazi.

Alisema lengo la ziara hiyo ni kupata tathmini ya awali ili kujua mafanikio na changamoto juu ya utaratibu wa uandikishaji na uhakiki wa taarifa za wapiga kura unavyoendelea.

Naye Afisa uandikishaji Wilaya ya Kaskazini ‘B’, Makame Pandu Khamis alisema zoezi la Uandikishaji wa Wapiga Kura Wapya na uhakiki wa taarifa za Wapiga Kura linaendelea vizuri katika vituo vyote vya Wilaya ya Kaskazini “A”.

Alisema zoezi hilo linaendelea vizuri kutokana na maandalizi na juhudi zinzochukuliwa na Watendaji wa Tume pamoja na Masheha wa Shehia kuhamasisha Wananchi wao kwenda katika vituo kujiandikisha na kuhakiki taarifa zao.

Aliongeza kusema kuwa, mpaka sasa Vituo vyote 33 vya Wilaya ya Kaskazini “A” pamoja na Vituo tisa vya Jimbo la Donge kuna Idadi Kubwa ya Wananchi waliojitokeza kuandikishwa na kuhakiki taarifa zao mbali na baadhi ya changamoto ndogo ndogo zilizojitokeza vituoni ambazo zilirekebishwa kwa kupewa maelekezzo wapiga kura kwenda katika vituo ambavyo zipo taarifa zao.

Alieleza kuwa amani na utulivu umetawala katika Vituo hivyo ambapo aliwataka wananchi hususan Vijana ambao wametimiza sifa za kuwemo kwenye daftari kwenda kujiandikisha na kwa wale waliokuwemo katika Daftari kwenda kuhakiki taarifa zao kwani bila kufanya hivyo hawatoweza kupiga kura kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Katika hatua nyengine Mkurugenzi wa Uchaguzi, Thabit Idarous Faina amewataka wananchi kuutumia vizuri muda kutokana na mfumo unaotumika kuandikisha wananchi na kuhakiki taarifa za Wapiga Kura unatumia muda mdogo sana wastan wa dakika moja mpaka mbili kwa mwananchi mmoja.

Alisema Tume ya Uchaguzi itamuandikisha kila mwananchi aliyetimiza sifa za kuandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar Nam. 4 ya mwaka 2018 ili kuweza kupiga kura katika Uchaaguzi Mkuu wa 2020.

Kwa upande wa baadhi ya wananchi waliiomba Tume ya Uchaguzi kaungalia uwezekano njia nyengine mbadala ya kuandikishwa katika daftari hilo badala ya kutumia kitambulisho kipya cha mzanzibar.

Facebook Blogger Plugin by Piere

Post a Comment

 
Top