Mamlaka ya Udhibiti wa
huduma za Maji, nishati na Mafuta Zanzibar ZURA imesema upungufu wa
mafuta ya Petroli uliojitokeza nchini katika vituo mbalimbali Zanzibar
unatokana na kuongezeka kwa mahitaji ya huduma hiyo kwa wananchi.
Akizungumza na
Zanzibar24 huko Ofisini kwake Maisara mjini unguja, Afisa Habari wa
Mamlaka hiyo Mbaraka Hassan Haji amesema kiwango cha mafuta
kilichotengwa kutumika kimekuwa kidogo ukilinganisha na mahitaji ya
wananchi hasa katika kipindi hichi cha skukuu ya mwaka mpya.
Amesema kampuni za
mafuta ikiwemo United Petrolium, Gapco huwaagiza mafuta kulingana na
kiwango cha matumizi wanachokihitaji katika bohari zao za kuhifadhia
mafuta lakini kiwango hicho kilizidiwa kutokana na mahitaji kuongezeka
zaidi kwa wananchi.
Aidha amesema kwa mwaka
huu mpya 2018 Mamlaka imeweka mikakati kuhakikisha tatizo la uhaba
wa mafuta linadhibitiwa ili lisiweze kujitokeza ambapo wameahidi
kukaa chini na makampuni ya mafuta yanayotoa huduma za mafuta visiwani
Zanzibar ili kushirikiana.
Hata hivyo amesema bado
mamlaka inakabiliwa na tatizo la sehemu ya kuhifadhia mafuta
kulingana na mahitaji lakini serikali imeshafanya hatua za kutafuta
eneo ambalo litatumika kwa ajili ya kuhifadhia mafuta ili liweze
kukidhi na kutoa huduma hiyo bila ya usumbufu wowote.
Chanzo, Zanzibar 24
Facebook Blogger Plugin by Piere
Post a Comment