Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amepewa onyo kali pindi akishiriki katika kampeni za uchaguzi za kumnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Kinondoni kupitia Chama cha Chadema na kuacha kumnadi mgombea waliyeteuliwa na Chama chake cha CUF katika Jimbo hilo.


Mkwala huo umetolewa na Kamanda Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF upande unamuunga mkono Profesa Ibahim Lipumba Thiney Juma ambaye aliibuka na kutoa kauli hiyo baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa huenda Maalim Seif akaibuka katika mikutano ya Chadema na kumnadi mgombea wa Chadema.


Thiney alisema kuwa pamoja na kuwepo kwa taarifa kuwa Maalim Seif huenda akamnadi mgombea huyo lakini atambue kuwa kufanya hivyo ni makosa makubwa kwa mujibu wa katiba ya CUF.


“Yeye ni kiongozi wetu mkubwa tu na anafahamu vizuri sana katiba ila tunasikia kama huenda akamnadi mgombea wa Chadema ila akisubutu kufanya hivyo kamati ya nidhamu lazima ichukue mkondo wake dhidi yake hasa kwa kuwa atakuwa amekiuka katiba yetu”alisema Thiney.


Thieney alisema kuwa kama Maalim Seif ana hamu ya kupanda jukwaani anaruhusiwa kupanda jukwaa la CUF katika Jimbo hilo hilo la kinondoni ambapo pia CUF nao wana mgombea wao katika kinyang’anyiro cha Ubunge.


Alisema kuwa hadi sasa wao kupitia vikao mbali mbali hawajachukua hatua yoyote ya kumtaka kiongozi huyo asishiriki kwenye kampeni za Chadema akisema kuwa Maalim Seif anajua wajibu wake kama kiongozi wa muda mrefu kwenye chama hicho.


“Maalim tunamtambua sana kama kiongozi wetu na ilipanswa yeye ndiye atongoze sisi sio sisi tumuongeze yeye katika hili la kukiuka katiba ya Chama chetu’alisema.

 Aliongeza kusema kuwa “Sisi tunashangazwa sana kuona kiongozi wetu huyo pamoja na kuwa na umri mrefu katika Chama lakini amekuwa ni mtu wa kushangaza kwa kufanya mambo yanayokwenda kinyume na katiba za Chama “alisema.


  
Alisema kuwa milango ipo wazi kwa Maalim kuachana kabisa na dhana yake hiyo akitambua kukaa pindi akithubutu kwenda kinyume na katiba ya Chama hatua za kisheria dhidi yake zitafuata bila ya kuoneana muhali.
 

Facebook Blogger Plugin by Piere

Post a Comment

 
Top