Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein ameitaka Kamati ya kombe la Mapinduzi Cup Zanzibar kushusha viwango vya kiingilio vya michezo hiyo kwa kuanzia alisema kuwa ianze kwa kiingilio cha elf moja au chini ya hapo.

Alisema kuwa kiwango hicho anaamini kitakuwa ni sababu moja wapo ya kumuwezesha kila mwananchi na mpenda soka kuingia kiwanjani humo ili kuangalia burudani safi ya michezo ya kombe hilo ambalo limeonekana kwua shauku kubwa kwa wananzchi ila kikwazo ni kiwango kikubwa cha kuingia kiwanjani humo.

Dk Shein aliyasema hayo leo katika kiwanjani cha Amaani katika bonanza maalum la michezo, ambapo alisema kuwa amepata malalamiko kutoka kwa wananchi kuwa kiwango kiliopo hivi sasa ni kikubwa wala hawawezi kukimudu ijapokuwa wana hamu ya kuangalia michezo hiyo.


Dk Shein alitumia fursa hiyo kwa kumtaka Waziri husika wa Michezo kuliangalia suala hilo na kulifanyia kazi mara moja akisisitiza kuwa kama kamati haina bajeti imuone ili kuangalia uwezekano wa kusaidiwa.


katika hatua nyengine Dk Shein katika risala yake ya kuaga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka 2018 amesema kuwa ni jambo la kufurahisha sana kwamba mwaka 2017 unaagwa huku Zanzibar ikiwa imeweza kuirudisha sifa na heshima iliyokuwepo miaka mingi katika mchezo wa Mpira wa Miguu.


Alisema timu hiyo  imeitangaza vyema Zanzibar katika Mashindano ya Kombe la  Chalenji la CECAFA kwa mwaka 2017.
Katika risala yake hiyo, Dk. Shein alisema kuwa Zanzibar imepata nafasi ya pili baada ya kufika fainali na kushindwa kwa njia ya penalti ambapo wachezaji wameonesha vipaji na uwezo wa hali ya juu.
“Wachezaji wetu wameonesha vipaji na uwezo wa hali ya juu na sisi tumeonesha mapenzi, mshikamano na uzalendo mkubwa kwa vijana wetu....Tumepata heshima kubwa katika mashindano haya”, alisisitiza Dk. Shein katika risala hiyo.
Aidha, Dk. Shein alieleza kuwa mafanikio hayo yaliopatikana ni ishara kwamba, juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar za kufufua michezo zimeanza kuzaa matunda mazuri.
Hivyo, Dk. Shein alitoa wito kwa wanamichezo na wananchi wote kushikiana katika kufufua na kuendeleza michezo hapa nchini.
Kwa mara nyengine tena, Dk. Shein alitoa pongezi maalum kwa wachezaji na viongozi wa Timu ya “Zanzibar Heroes” kwa mafanikio makubwa iliyoyapata timu hiyo na kupelekea kuiwakilisha na kuitangaza vyema Zanzibar kitaifa na kimataifa.
Vile vile, Dk. Shein alitumia fursa hiyo kutoa pongezi kwa vijana wa “Zanzibar Sand Heroes”(Mashujaa wa Mpira wa Ufukweni) kwa kufika fainali na kuifunga timu ya Malawi magoli matatu kwa mawili na kuchukua kikombe cha mashindano hayo.
Dk. Shein alisisitiza kuwa nayo timu hiyo imeiletea sifa kubwa Zanzibar kwa mara ya kwanza kutokana na ushindi wake huo.
Pamoja na hayo, Dk. Shein aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika mashindano maalum ya mpira ya kombe la Mapinduzi (Mapinduzi Cup) pamoja na Michuano ya “ZBC Watoto Mapinduzi Cup” ambayo yanazishirikisha timu za watoto wa Wilaya zote za Unguja na Pemba.
Sambamba na hayo, Dk. Shein aliwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi katika Tamasha la nne la maonesho ya biashara litakaloanza rasmi tarehe 7 hadi 16 Januari 2018 kwenye viwanja vya Maisara.
Dk. Shein pia, aliwataka wananchi wahakikishe kwamba kila mtu anapata fursa ya kuyaona maonesho hayo huku akiwataka kujitahidi kuhudhuria katika kilele cha Sherehe za Mapinduzi zitakazofanyika katika uwanja wa Aman tarehe 12 Januari, 2018. 

Facebook Blogger Plugin by Piere

Post a Comment

 
Top