Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imepokea ujumbe kutoka Kampuni ya Kimataifa ya China ijulikanayo kama ‘China National Offshore Oil Corporation (CNOOC)’ inayojishughulisha na uchimbaji wa Mafuta na Gesi asilia.

Viongozi wa Kampuni hiyo wamefika katika Wizara ya Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira Zanzibar huko Forodhani Mjini Unguja na kufanya mazungumzo na wenyeji wao ikiwa ni miongoni mwa utekelezaji wa makubaliano yao juu ya suala la mafuta na gesi asilia visiwani humu .


 Akizungumza kuhusu ziara ya ujumbe huo wa (CNOOC) visiwani humu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira Zanzibar, Ali Khalili Mirza alisema ujumbe huo ni utekelezaji wa makubaliano ambayo Kampuni hiyo ilitiliana saini na Serikali ya Mapunduzi ya Zanzibar mwaka jana juu ya suala la mafuta na gesi asilia.

“Uongozi wa kampuni hii ambayo ni kubwa katika anga za masuala ya mafuta duniani hasa katika utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi imetuma viongozi wake hawa kwa lengo kudumisha ushirikiano kati yao na Serikali yetu ya Mapinduzi Zanzibar”alisema .

Mizrai alisema kuwa kazi kubwa ya kampuni hiyo visiwani hapa kwa hatua ya kwanza itaanza na utoaji wa mafunzo kwa wafanyakazi mbali mbali wa masuala ya mafuta mafunzo ya muda mfupi na mrefu wakiwa chini ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

“ Katika hati yetu ya makubaliano tuliyoweka kati yetu na kampuni hiyo ni  inaonesha kuwa pamoja na kazi nyengine lakini pia viongozi hao watapata nafasi ya kutoa mafunzo ya kwa wataalamu wa Zanzibar wataoshughulika na sekta ya Gesi na Mafuta”alisema Mizrai.

Aidha Wataalamu hao kutoka Zanzibar pia watapata nafasi ya kwenda nchini China kupata mafunzo zaidi kuhusiana na Mafuta na gesi asilia.

 “ kampuni ya (CNOOC) imeweza kuonana na Waziri na wamekuja hapa kuweza kusalimiana nae kama nyumbani na baadae wataweza kuonana na viongozi mbali mbali wanaohusika na sekta ya Mafuta na Gesi ”alisema Katibu Mkuu.

Kuhusu hatua ya uchimbaji wa Mafuta iliyofikiwa hapa Zanzibar Katibu Mirza alisema bado suala hilo lipo katika hatua ya utafiti na kwamba Wataalamu watakapomaliza taarifa ya matokeo ya utafiti itatolewa kwa Wananchi.

Facebook Blogger Plugin by Piere

Post a Comment

 
Top