Wafanyabiashara  wanaoingiza bidhaa nchini Zanzibar  kutoka nchi mbalimbali wametakiwa  kufuata  sheria na taratibu zilizowekwa  za uingizaji wa biashara ikiwemo  kuzisajili bishaa na kufanyiwa uchunguzi  kabla hawajazisambaza sokoni  ili kumlinda mtumiaji kutopata madhara.

Akizungumza na wakala wa forodha na wafanyabiashara wa chakula,dawa,vipodozi  na vifaa tiba Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa  chakula,dawa,vipodozi na vifaa tiba Zanzibar katika ukumbi wa mkutano  Kidongo chekundu mjini Unguja  Burhani Othman Simai amesema  kupitia sheria  namba 3 ya chakula,dawa na vipodozi  itaweza kusaidia katika kudhibiti  wafanyabiashara kuingiza bidhaa nchi zisizo na  ubora na viwango kwa watumiaji.

Amesema  imebainika  kuwepo kwa wafanyabiashara  kukiuka  taratibu  zilizowekwa  na serikali nchini ya taasisi hiyo ya wakala wa chakula dawa na vipodozi  kwa kuingiza bidhaa zisizostahiki  na kupelekea athari  mbalimbali wa wananchi wa Zanzibar ambao ni watumiaji wakubwa.

Hata hivyo Burhani amesema Wakala  hatokubali kuona nchi inaingizwa bidhaa zilizombovu  lazima  zifanyiwe ukaguzi na  kusajiliwa  kabla ya kutumiwa  ili  bidhaa zote zinazoingizwa ziwe na ubora  kuanzia viwandani.

Kwaupande wao baadhi ya Wafanyabiashara hao wakizungumza na Zanzibar24 wameziomba  taasisi zinazohusika na udhibiti wa ubora wa bidhaa ikiwemo ZBS,Mkemia mkuu na Wizara ya Afya kuandaa sheria  watakayoitumia pamoja ili  kuondoa migongano  ya kisheria  wao na wafanyabiashara wanaoingiaza  bidhaa nchini.

Wamesema  nivyema sasa serikali kujipanga  kuzifanyia maboresho  maabara zao za ukaguzi wa bidhaa kuweza kufanya kazi  kwani imeonekana kutokuwa na uwezo  katika utendaji ndio maana wafanyabiashara wengi hukwepa kupeleka bidhaa zao na kutafuta maabara ambazo wataona zina mapato Sokoni.

Mkutano huo wenye lengo la kuwatambulisha  wafanyabiashara mabadiliko  ya mfumo wa kiuchumi  kutaka bidhaa zote zipate ithibati za kimataifa ili kuingia katika masoko makubwa ya kimataifa.
chanzo, Zanzibar 24

Facebook Blogger Plugin by Piere

Post a Comment

 
Top