Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu na Uwekezaji Doroth Mwaluko amesema kufanyika Mkutano wa Kamati ya Mawaziri wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika  (SADC) kutasaidia kubadilishana taarifa za uzoefu pamoja na kupunguza athari za Maafa .
Hayo aliyasema wakati wa Kikao cha Makatibu Wakuu na Maafisa Waandamizi huko katika Ukumbi wa Madinat Al- Bahr Mbweni Zanzibar
Alisema kikao hicho kitasaidia kuwa na jukwaa la kubadilishana uzoefu wa kiutendaji kwa lengo la kutekeleza kwa ufanisi shughuli za usimamizi wa maafa
Aidha alisema Mkutano huo umekuja katika kipindi ambacho nchi nyingi wanachama katika ukanda huu zimekuwa zikiathiriwa na majanga ya asili ya mara kwa mara na kusababisha madhara makubwa .
Nae Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Abdalla Hassan Mitawi amezishauri Nchi wanachama wa SADC kushirikiana katika kukabiliana na maafa kwa hatua watazozichukua ili kudhibiti athari za kimazingira zinazoweza kujitokeza.
Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tayari inatumia boti za uokozi pamoja na ndege zisizokuwa na rubani kwa kuimarisha shughuli za uokozi hata hivyo inahitaji ushirikiano unahitajika kutoka Nchi nyengine.
 Mkutano huo wa Ngazi za Makatibu Wakuu unaandaa Ajenda zitazojadiliwa katika Mkutano wa Mawaziri unaotarajiwa kufunguliwa siku ya Ijumaa ijayo na Mgeni Rasmi wa Mkutano huo ni Rais wa ZanzIbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein katika Hoteli ya Madinat Al Bahr
Kauli mbiu ya mkutano huo ni “USHIRIKI WA KISEKTA KWENYE KUPUNGUZA MADHARA YA MAAFA NI NJIA BORA YA KUIMARISHA USTAHAMILIVU KATIKA UKANDA WA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA MAENDELEO KUSINI MWA AFRIKA” ( SADC)
 Mkutano wa Kwanza wa Kamati ya Mawaziri wenye dhamana ya uongozi wa  Maafa kwa Nchi Wanachama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) kwa  Nchi Wanachama 15 kati ya 16 zitashiriki Mkutano huo .

Facebook Blogger Plugin by Piere

Post a Comment

 
Top