Mpaka sasa miili zaidi ya 125, imepatikana katika ajali ya kivuko cha MV. Nyerere kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella na zoezi la uokoaji linaendelea

Saa 6:40 Mchana, Septemba 21: Jeshi la Polisi kufungua Jalada la uchunguzi
Mkuu wa Jeshi la Polisi, Nchini (IGP) Simon Sirro amesema kuwa litafunguliwa Jalada maalum la kuchunguza tukio la kuzama kwa kivuko cha MV. Nyerere jana, Septemba 20 mita chache kabla ya kuwasili katika kisiwa cha Ukara.

IGP Sirro amesema kuwa kwa sasa zoezi la utambuzi wa miili iliyopatikana linaendelea huku pia uokoaji ukiendelea ili kutafuta wengine ambao hawajapatikana.

Facebook Blogger Plugin by Piere

Post a Comment

 
Top