Waziri wa Habari Utamaduni na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo amesema Vyombo vya Habari na Waandishi wa Habari wanajukumu la Kufanya kazi kwa kufuata sheria na maadili ya kazi zao ili kuiweka Nchi katika hali ya Amani na Usalama.

Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru ya Vyombo vya Habari yaliyofanyika  katika Ukumbi wa wizara ya Habari Kikwajuni Mjini Zanzbar amesema Vyombo vya Habari na Waandishi  wanategemewa sana katika jamii hivyo si vyema  kufanya kazi kinyume na maadili yao.

Amesema  watakapoendelea kufanya kazi kwa sheria  watawawezesha wananchi Kunufaika na haki zao za Msingi na serikali kuweza  kutoa huduma Muhimu katika jamii zitakazoimarisha Maendeleo ya Nchi.

Amesema  kutokana na umuhimu wao Serikali pia itaendelea kuthamini   na Kuheshimu Uhuru wa Vyombo vya Habari pamoja na kuendelea kutoa  taarifa zinazohitajika  ili kuwawezesha Waandishi kufanya kazi zao kwa weledi.

Aidha ametowa wito kwa waandishi wa Habari kuripoti Sehemu Husika matatizo wanakutana nao wakati wa utendaji wa kazi zao ikiwemo  tatizo la mikataba baina yao na waajiri wao ili matatizo hayo yaweze kupatiwa ufumbuzi.

Awali Raisi wa Clabu za Waandishi wa Habari Nchini Tanzania Deogratius Nsokolo amesema licha ya Waandishi wa habari kufanya kazi kwa Kufuata Sheria lakii wamekabiliwa na Matatizo mbalimbali ikiwemo  kukosa Mikataba,bima za Afya na Mafao katika Tasisi zao.

Amesema ili Mwandishi wa habari aweze kufanya kazi kwa kuwafikia wananchi ni vyema kwa Vyombo vya Hbari kujali Afya na Mahitaji ya Wandishi wa habari ili Vyombo hivyo viweze kufikia malengo waliyoyakusudia.

 

Aidha ametowa wito kwa Waandishi wa Habari kuendelea kufanya kazi kwa kwa mashirikiano katika kuwasaidia wananchi kwa kuwakosoa na kuwakumbusha viongozi wa Serikali kujua wajibu wao juu ya kutatua matatizo yanayowakabili Wananchi.

 

Facebook Blogger Plugin by Piere

Post a Comment

 
Top