Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein leo
amewaapisha Mawaziri pamoja na baadhi ya viongozi aliowateua jana kushika
nyadhifa mbali mbali katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Hafla
hiyo ilifanyika Ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa
Serikali akiwamo Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi, Mwanasheria Mkuu
wa Zanzibar,Said Hassan Said, Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu , Spika
wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid.
Viongozi
wengine waliohudhuria ni Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih, Kadhi
Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji, Wakuu wa Vikosi vya SMZ, Washauri wa Rais
wa Zanzibar pamoja na viongozi wengine wa Serikali.
Mawaziri
walioapishwa ni Waziri wa Biashara na Viwanda, Balozi Amina Salim Ali, Waziri
wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo Balozi Ali Abeid Karume, Waziri wa
Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji, Dk Sira Ubwa Mamboya.
Wengine
ni Waziri wa Afya, Hamad Rashid Mohamed, Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na
Uvuvi, Rashid Ali Juma, Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati, Salama Aboud
Talib, Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale, Mahmoud Thabit Kombo, Waziri
wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto, Maudline Cyrus Castico.
Manaibu waliapishwa ni Naibu Waziri wa Ardhi,
Nyumba, Maji na Nishati, Juma Makungu Juma, Naibu Waziri wa Habari, Utalii na
Mambo ya Kale, Choum Kombo Khamis, Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee,
Wanawake na Watoto, Shadia Mohamed Suleiman, Naibu Waziri wa Kilimo, Maliasili,
Mifugo na Uvuvi, Dk Makame Ali Ussi, Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda Hassan
Khamis Hafidh.
Dk
Shein pia aliwaapisha Wakuu wa Wilaya aliowateua hapo juzi ambao ni Issa Juma
Ali aliapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Pemba na Rajab Ali Rajab kuwa Mkuu
wa Wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja.
Viongozi
hao walioapishwa kwa pamoja waliahidi kuendelea kumsaidia Rais Dk Shein katika
kuhakikisha Zanzibar inazidi kupata maendeleo kama ilani ya Chama cha Mapinduzi
inavyosema.
“Tunaendeleza
kuimarisha mashirikiano ya dhati katika kuwatumikia wananchi, kuleta mabadiliko
na kufanya kazi kwa vitendo sambamba na kuendelea kusimamia amani na utulivu
uliopo nchini” walisema .
Hatua
hiyo imekuja baada ya jana Dk Shein kufanya mabadiliko madogo katika Baraza la
Mapinduzi kwa kuongeza Wizara moja zaidi na kuwabadilisha Wizara baadhi ya
Mawaziri.
Kufuatia
mabadiliko hayo, shughuli za Vijana zimehamishiwa katika Wizara mpya ya Vijana,
Utamaduni, Sanaa na Michezo shughuli za Mazingira zimehamishiwa katika Ofisi ya
Makamu wa Pili wa Rais na shughuli za Wakala wa Serikali wa Uchapaji
zimehamishiwa Wizara mpya ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale.Aidha.
Dk
Shein pia amewateua Naibu Mawaziri wapya wawili na kumbadilisha Wizara Naibu
Waziri mmoja ambapo kufuatia mabadiliko hayo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
hivi sasa itakuwa na Wizara 14 badala ya 13 za hapo awali .
Facebook Blogger Plugin by Piere
Post a Comment